Tuesday, 29 July 2014

INSHA MUFTI AND AWESOME COMPOSITION: JINSI YA KUANDIKA INSHA MUFTI

INSHA MUFTI AND AWESOME COMPOSITION: JINSI YA KUANDIKA INSHA MUFTI




Miaka Kumi Baadaye, Nakukumbuka Babangu!

Tarehe kamili kama leo miaka kumi iliyopita, jambo lililobadili maisha yangu
kabisa lilitokea. Asubuhi Desemba tarehe 2 2001, nilijinyanyua kwenda
kufunga mfereji wa maji uliyokuwa ukichuruzika usiku kucha. Baba alikuwa
amenikumbusha kuufunga vyema kabla kulala ili maji yatakapofunguliwa
usiku katika bomba kuu la jengo letu, yasipate kumwagika. Ni agizo
ambalo nilisahau kutimiza na hivyo kulazimika kuamka alfajiri na mapema
saa kumi na moja kwenda kuzima. Kibaridi kisicho cha kawaida kilinipiga
mwilini na kunifanya kuganda. Nilihisi kuwa kuna jambo lisilo la kawaida
linalonitendekea lakini sikujua ni wapi au vipi.


Nilihofia manake nilidhani nitampata baba ameamka kama ilivyokuwa
desturi yake ili ajitayarishe kwenda kazini. Laiti ningalijuwa
yaliyonisubiri! Nikakwenda mlangoni mwa chumba alimolala baba na kubisha
mlango kwa upole. Baba! Baba! Baba! Niliitana lakini sikupata jawabu.
Jambo ambalo halikuwa la kawaida.


Kwa utaratibu mkubwa niiliiufungua mlango na kuingia. Nikanyatia
kitandani alikolala baba na kuanza kumtikisa huku nikimwita. Niliona
kuwa alikuwa amechelewa kuamka ili kujitayarisha kuenda kazini na iwapo
angeendelea kulala hivyo basi angechelewa kufika kazini.


“Baba! Amka baba wakati umefika” masikini niliitana nisipate jibu.
Jambo lililonipa msukumo wa kumfunua. Lo! Baba alikuwa amelala kwa
utulivu na kuunyosha mwili wake kabisa. Alikuwa kasha lala usingizi
usiojuwa wakati wake wa kuamka. Kama mchezo tena kwa ghafla, babangu
mzazi alikuwa ameaga katika usingizi wake. Niliona dunia yangu
ikizunguka na macho karibu yanitoke maanake sikujua pa kuanzia. Asubuhi
na mapema vile, na umri wangu mdogo wa miaka kumi na mitatu  tena katika
darasa la saba, ningeanzia wapi ilhali familia yetu ilikuwa katika mji
tofauti na mimi ndiye niliishi na baba? Ilikuwa mwaka wa 2001.
Yaliyofuatia yalibaki kitendawili kwani sikuwahi amini ya kuwa baba
yangu alikuwa ameaga hadi mwaka wa 2005!


Sasa
napiga darubini yangu nyuma, mengi yamejiri mno katika familia yetu
ambayo sina budi kumshukuru Maulana kwa majaliwa yake. Ndiye Mungu
mwenye kutujalia neema ndogondogo na neema kubwa kubwa. Babangu
akifufuka leo, atashtuka kumpata mwanawe wa kwanza alijitaidi masomoni
hadi kukamilisha chuo kikuu na kwa sasa ninachapa kazi! Ajabu maanake
aliniwacha katika darasa la saba wakati hata masomo ya msingi sikuwa
nimemaliza.  Wenzangu wanaonifuata pia wamejitahidi na kuingia katika
vyuo vikuu na wengine kukamilisha masomo ya sekondari.


Zaidi ya  yote, daima namshukuru mamangu mzazi. Amekuwa kipa imara
kwetu katika miaka hizi zote na kutia bidii kama za mchwa kuwapa wanawe
maisha bora. Isingalikuwa mamangu, nisingelikuwa nilipo. Amekuwa mnara
wetu nyakati zote! Alinipa tabasamu na sababu ya kuona siku mpya hata
nilipodhani kuwa yote yamekwisha.


2 comments: