MAUTI YALIBISHA MLANGONImauti yalibisha

Mogiri alifungua mlango polepole na kutoka nje. Alinikuta nimeketi kwa
fomu ndefu hapo nje ya wodi nikisubiri. Nilikuwa nimejishika tama na
kuzama katika luja ya mawazo. Ni kweli kwamba mshika tama huwa analo
moyoni.nilimwangalia kwa macho ya atiati nikitazamiakusikia mengi
kumhusu mke wangu Zuhura. Sikujua kilichomtendekea tangu aingizwe mle
ndani ya chumba cha upasuaji, masaa matano yaliyopita. Kumbe kweli
usilolijua ni kama usiku wa manane.
Akilini mwangu, yaliyotendeka yalikuwa yangali mbichi mno. Nilitoka
kazini mapema alasiri hiyo na kurudi nyumbani kwani sikuwa na kazi
nyingi ya kufanya. Nikafululiza hadi mlangoni na kubisha bila kupata
jibu.wanenao husema kuwa kimya kingi kina mshindo. Nilifungua mlango
polepole na kuingia ili kugundua kilichonisubiri. Lo! Ukistaajabu ya
musa utayaona ya firauni.
Zuhura alikuwa kalala sakafuni, akigaaga na kufurukuta kwa uchungu na
kutoa sauti ya maumivu. Aliye na macho haambiwi tazama. Nilielewa fika
kuwasiku zake za kujifungua zilikuwa zimewadia. Kasha akajikazana
kutamka,
“Nisaidie jamani.” Kisha akanyamaa ghafla na kuendelea kufurukuta.
Fimbo ya mbali haiui nyoki kwa hivyo, niliwaita majirani walionipa
usaidizi wa kutafuta rukwama ili kumpeleka hospitalini. Ilikuwa nadra na
adimu kama wali wa daku kuona magari katika sehemu tuliyoishi. Sehemu
ya Ngomani. Kama wakaazi wa pale, tulizoea maisha hayo na haikuwa ajabu
kumwona akipanda au kuabiri ‘gari’ letu- rukwama. tulimpeleka kwa
zahanati ya kipekee hapo mjini na kupata kuwa muuguzi hakuwepo. Nikawa
nimechanganyikiwa nisijue la kufanya jirani mmoja aliposhauri
tumkimbize Zuhura katika hospitali ya wilaya.
Hospitali ya Afueni ilijulikana kote kwa kuwa ya bei ghali. Lakini
nilishawishika na kukubali kwani maisha ya Zuhura ilikuwa muhimu kuliko
pesa. Tukaandamana hadi kule. Hisia za uchovu na kutamauka tayari
zilianza kuninyemelea nikawa nafuata wenzangu tu kama bendera
inavyofuata upepo au maji inavyofuata mkondo. Moyo wangu ulijaa ukunjufu
kwa ukarimu walionionyesha.

nimeketi hapo nikisubiri matokeo ya daktari waliokuwa wakimhudumia.
Takribani miaka mine sasa tangu tufunge ndoa, Zuhura alibaki tasa
asiweze kupata motto hata mmoja. Mara nyingi nilimsikia akimlilia Muumba
wake na kusali. Hatimaye maombi yake yalijibiwa na sasa tulikuwa
tukitarajia mwana wetu wa kwanza. Tayari nilikuwa na cheche za
matumaini. Penye nia pana njia eti. Hata nikakisia kuwa atakuwa msichana
na tungemwita Zawadi. Pengine kama ishara kuwa Maulana alitupa zawadi
baada ya miaka. Nilisahau kabisa onyo la wahenga eti usikate kanzu kabla
motto hajazaliwa.
Daktari Mogiri akanisongelea na tukaanza majadiliano. Mazungumzo ya
kiume kama alivyoyataja. Mara kwa mara niliwaona wauguzi wakipitapita
kushoto-kulia wakiendelea na shughuli zao. Daktari alikuwa amemaliza
kazi yake muhimu mle ndani.
“Unatarajia mtoto wa jinsia ipi? Mbona? Mtamwita nani? Utampa Zuhura
zawadi gain kwa kazi aliyofanya?” aliniuliza maswali chungu nzima.
Maswali yenyewe yakatuongoza katika ulimwengu wa gumzo. Tukazungumza na
kupitiza wakati bila hata kugundua. Hata chembechembe za wasiwasi
nilizokuwa nazo zikanitoka kabisa. Nikajihisi huru, kiumbe mpya na
nikavaa piku la tabasamu.
Ndipo sasa daktari akaamua kunipasulia mbarika hatimaye. Akanidokezea
kuwa Zuhura alikuwa amejifungua motto wa kiume mwenye buheri wa afya.
Singejizuia tena.licha ya kuwa
usiku ulikuwa umeingia, nilirukaruka kwa furaha kupindukia ungedhani
mwenda wazimu. Nikatamani majirani wote waliomleta Zuhura wangalikuwepo
lakini walikuwa washarudi makwao kushughulikia jamii zao. Nikaanza
kuwazia jina la motto wetu nikiwa katika hali ya kurukaruka
bado. “Tutamwita Bahati”
Nilisema kwa nguvu huku nimemkumbatia daktari kwa furaha macho yangu
nikiwa nimeyafumba.
Daktari alikuwa akinitazama tu kwa wakati wote huo pasi na la kusema.
Lakini nilipoanza kuuelekea mlango wa chumba alimolazwa mke wangu,
alinisitisha na kunizuia. Akaniomba kusubiri lakini furaha iliyonijaa
ikanifanya kuwa kiziwi. Nikajitia pamba masikioni nisisikie la mwadhini
wala la mteka maji msikitini.
Akanivuta kando kidogo na kunidokezea kuwa Zuhura mwenyewe alifuja na
kupoteza damu nyingi hivyo basi asingeweza kuishi! Kwa kifupi,
aliniambia kuwa mke wangu alikuwa amea…sikuyaamini macho na masikio
yangu. Maneno hayo yalinifanya kiuwa chakaramu zaidi. Yalinikata maini,
yakanikera na kunikereketa ajabu. Uso wangu uliokuwa na furaha
ulibadilika ghafla na kufinga. Kwa nguvu kama za tembo na hasira za
mkizi, niliuendea ule mlango bila kumjali yeyote wala chochote.
Alinifuata na kujaribu kunivuta nyuma huku akiniliwaza. Juhudi zake
zikangonga mwamba.
Sikujua kuwa daktari ni watu wenye vipawa vha kuwapumbaza watu namna
hiyo! Kwa muda wote huo, daktari alikuwa amejua ukweli na kunificha kwa
kunishirikisha katika mazungumzo. Pengine hayo ni baadhi ya mafunzo
wanayopewa wanaposomea fani ya udaktari lakini ubunifu wa ya Mogiri
ulishinda wote. Niliajabia ubunifu wake!
Niliingia kwa fujo na rabsha kama mfungwa aliyeachiliwa huru. Wauguzi
wakashtuka na kujaribu kunizuia. Daktari akaingia na kuagiza nionyeshwe
mtoto. Nikaelekezwa hadi alikokuwa. Mtanashati ajabu na mwenye afya
ungedhani kutoka mbinguni. Alilala kwa utulivu asijue mamake alikokuwa.
Laiti angejua. Lakini kuonyeshwa mtoto haikunisaidia wala kinutuliza.
Nani angekilisha,akivishe na kukilinda siku zote? Unyama upi huo
kuingizwa katika ulimwengu na kuachwa na mwenyeji wako hata kabla ya
kumwona ana kwa ana? Nilijihurumia, nikamhurumia malaika wa Mungu.
Machozi yakanidondoka kama mtoto na nikayaacha kumwagika bila aibu.
Kwa mwongozo wa daktari, nilifululiza hadi alikolazwa Zuhura.
Msichana mrembo aliyeumbwa akaumbika alikuwa amelala kwa upole na
utulivu asijue hata wakati wa kuamka. Alikuwa amefunikwa vizuri hata
usingedhani ni maiti. Ikanifanya kutoamini na kuanza kumwamsha. “Zuhura,
amka umwone Bahati mwana wetu.”
Akawa haoni, hasemezi,hatikisiki. Kimya kikajiri. Niliinama kando
yake na kumtikisa tena mara hii kwa nguvu machozi zaidi yakinitoka.
Nikamshauri ainuke twende kwetu tusherehekee kuzaliwa kwa mtoto wetu.
“Zuhura” niliita mara ya mwisho kwa nguvu na pumzi ikaniishia.
Sauti nyororo ya Zuhura aliyekuwa amelala kando yangu usiku wote
ilinigutusha kutoka usingizini ikinijuza kuwa kumekucha. Miale ya jua
nayo ilikuwa imeshachomoza nje. Furaha iliyoje kupata kuwa hiyo ilikuwa
ndoto ya ajabu.
No comments:
Post a Comment