MDUDU ALINIUMA

jua lilikuwa limemaliza kazi yake na sasa lilijikokota magharibi huku
mionzi yake miekundu ikiwapungia walimwengu kwa ulegevu kana kwamba
kuwashukuru wale wote walioipenda. Masikini nilibaki pale uani
nimelitumbulia macho, huku machozi yakijikusanya tayari kumwagika. Heri
ningekuwa jua. Nisingekuwa na wasiwasi wa swala lolote. Langu lingekuwa
tu kuchomoza asubuhi na kutua jioni.
Nilikuwa nimechoka kuwatazama wapita njia na magari ya kifahari.
Yalikuwa mapya na yalikwenda kwa kasi tena bila kutoa sauti. Lakini kuna
yale yaliyochakaa yenye breki zilizokwaruzana kila yaliposimama. Watu
nao walipita wa aina tofautitofauti; si weusi, si weupe, warefu kwa
wafupi na hata vijana kwa wazee. Kwa umbali,taa za umeme zilikuwa
zimelimwaia jiji mchana bandia wa mwangaza. Ishara kuwa usiku ulikuwa
unaingia na giza kuanza kutawazwa.
Yote hayo sikuyaonea fahari tena. Mambo yalikuwa kangaja kumbe na
sasa yalikuja. Niliketi nikiwazia matokeo ya daktari, ambayo niliyapokea
takribani miezi miwili iliyopita. Awali, walinificha ukweli lakini
niliposisitiza, nilipasuliwa mbarika. Laiti wasingelinijuza kwani tangu
hapo maisha yangu yalichukua mkondo tofauti mno. Mwenyewe, ile hamu na
tama ya kula vyakula iliniondokea. Nikawa sili lolote, sinywi chochote.
Mashavu yangu yalizidi kushobwekea ajabu. Nguo zangu ningezivua, mbavu
zingehesabika hadharani moja baada ya nyingine. Nyele zangu zilizokuwa
ndefu na nyeusi ti sasa zilibadili rangi na kuanza kuchipuka ovyoovyo.
Mdudu alikuwa ameniuma. Lakini yupi?
Darubini yangu ilinikumbusha mambo yalivyoanza. Yote yaling’oa nanga
baada ya kumaliza kidato cha nne. ‘Mrembo’ nilijidai kwenda jijini
kutafuta kazi ya ukarani. Niliwahakikishia wazazi kuwa nilikuwa na
rafiki wengi waliojitolea kunipa makao wakati nikitafuta kazi. Wavyele
wakadinda kuniruhusu mwanzoni lakini baada ya kuzidi kusisitiza na
kufanya kiburi nyumbani, waliafikiana na kuniacha kwenda zangu. Pengine
walikumbuka kuwa mtoto akililia wembe mpe. Nilipokuwa nikiondoka, mama
alikuwa na huzuni mno na kwa uchungu, alinionya kuwa mwenda tezi na omo
marejeo ni ngamani. Potelea pote. Sikutaka kusikia ya yeyote kwani
nilijitia hamnazo nisikie la mwadhini wala la mteka maji msikitini.
Nikawa binti kiziwi asiyesikia anayoambiwa.
Kazi baada ya kuikosa,nilijiunga na wenzangu na tukajiajiri wenyewe.
Malipo yakawa ya kuvutia ajabu kwani wateja walivyoongezeka ndivyo
malipo yalivyoongezeka. Alimradi ujue namna ya kuwaongelesha na
kuwahudumia wateja sawasawa. Jambo ambalo nilijifunza kufanya hata
nikabobea na kutopea katika nyanja hiyo. Waume niliwabadili kama
nilivyobadili mavazi yangu kwa siku. Nikawa ndiye jogoo la shamba
lililowika jijini. Nikazika katika kaburi la sahau kuwa jijini kuna papa
na papaupanga, ambao ukiwapapia, hukosi kupapatika kwa majuto, dhiki na
mateso kama hayo yaliyonikumba sasa. Lau kumbe mwiba wa kujidunga hauna
kilio.
Kutoka hapo uani nilikoketi, taa za umeme nilizoziona zilinikumbusha
mengi. Kuhusu mienendo yangu ya awali nilipokuwa kipusa ajabu. Niliingia
kwa vilabu hivyo vyote vya usiku huku mikono ya watu tofauti yamezinga
kiuno changu chembamba kama cha nyigu. Daima kucha zangu zilizokuwa
ndefu na zilinaksishwa rangi sawia na nguo zilizovalika. Mdomo wangu
ukakolezwa rangi nyekundu kana kwamba nililamba damu mbichi. Lakini
kumbe dunia mti makavu kiumbe usiuegemee.
Watu hao niliowatazama waliniongezea uchungu mtupu. Moyo wangu
mchanga ulijaa uchukivu na furaha ikawa imeyeyuka kama kipande barafu
katika utupu wa mchanga wa jangwa la Sahara. Wale wasichana warembo
waliovalia mavazi yaliyoacha sehemu za miiliyao kuonekana waliniudhi
zaidi. Laiti wangelijua kuwa dunia itawararua na kuwaacha uchiuchi,
wasingefika hata barabarani. Nilitamani kuwafikia niwaonye na kuwapa
ukweli wa mambo kuhusu madhara ambayo yangewasibu lakini nilishindwa.
Mimi pia nilikuwa hivyo na sasa nilikuwa naangamia. Nikakumbuka kuwa
asiyefunzwa na mamake hufunzwa na ulimwengu.
Waume nao niliwatazama kama wanyama mwitu waliovalia suruali ndefu na
sharti tofauti. Wanyama wenye uwezo mkali wa kukuvamia wakakumaliza
kabisa. Wao ndio walionipa maji machafu yaliyokuwa na mdudu ambaye
aliniuma na kunifanya kuugua sasa. Niliwatazama kwa uchukivu mwingi.
Raha nyingi ya ulimwengu ulitoweka na badala yake ikawa sasa ni
huzuni tupu na majuto. Sasa niliishi kwa jumba hilo kubwa peke yangu.
Ulimwengu ulinitenga kana kwamba mwenye ukoma. Wale wote waliokuwa
wakiingia na kutoka siku nzima hata usingewaona. Dada yangu mdogo ndiye
alijitolea kuniuguza pale kwani sikutaka kuishi na wazazi na kuwapa
mzigo wa kunitunza. Ikanijia kuwa mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.
Sikujua wa kumlaumu. Wazazi? La wao walinitakia mema na kunionya kusoma
kwa bidii. Marafiki? Kwa kiasi kidogo lakini ndimi niliyekubali
kudanganywa. Ulimwengu? Ndiyo lakini sehemu gani ya ulimwengu? Mimi
ndiye wakulaumu na sasa mwiba wa kujidunga hauna kilio.
Ndoto zangu zote zilitoeka kama ukungu na umande. Azimio langu la
kutaka kuendeleza masomo katika chuo kikuu katika fani ya sheria, na
kufuzu katika uzamifu na uzamili lilitoweka ghafla kama mwangaza wa
mshumaa uliozimwa na upepo. Nilitoka uani na kuingia katika chumba
changu cha kulala. Mezani, kulikuwa picha yangu ya awali.nilijiangalia
tena na kujiona tofauti; mnene, mwenye sura ya maji ya kunde tena
mcheshi ajabu. Lakini sasa nilikuwa kama shetani hata ingawa sijawahi
kuonana naye ana kwa ana. Haina maana kuishi katika hali hiyo!
Niliifikia kalamu na kuandika kitu kwa karatasi iliyokuwa hapo kando.
Kasha nikavuta kijichupa kilichokuwa hapo juu na kupiga makopo kadhaa ya
yaliyokuwemo. Maini ya kaanza kukeketeka na koo kuungua ndanindani.
Heri nife niiondokee dunia. Safari yangu ya kuenda jongomeoni ikawa
imeanza nilikolala sakafuni.
Niligutuka usingizini nikihema na kutweta kwa nguvu mno hata nikashindwa kuendelea kulala. Ilikuwa ndoto ya ajabu.
Yalikuwa mapya na yalikwenda kwa kasi tena bila kutoa sauti. Lakini kuna
yale yaliyochakaa yenye breki zilizokwaruzana kila yaliposimama. Watu
nao walipita wa aina tofautitofauti; si weusi, si weupe, warefu kwa
wafupi na hata vijana kwa wazee. Kwa umbali,taa za umeme zilikuwa
zimelimwaia jiji mchana bandia wa mwangaza. Ishara kuwa usiku ulikuwa
unaingia na giza kuanza kutawazwa.
Yote hayo sikuyaonea fahari tena. Mambo yalikuwa kangaja kumbe na
sasa yalikuja. Niliketi nikiwazia matokeo ya daktari, ambayo niliyapokea
takribani miezi miwili iliyopita. Awali, walinificha ukweli lakini
niliposisitiza, nilipasuliwa mbarika. Laiti wasingelinijuza kwani tangu
hapo maisha yangu yalichukua mkondo tofauti mno. Mwenyewe, ile hamu na
tama ya kula vyakula iliniondokea. Nikawa sili lolote, sinywi chochote.
Mashavu yangu yalizidi kushobwekea ajabu. Nguo zangu ningezivua, mbavu
zingehesabika hadharani moja baada ya nyingine. Nyele zangu zilizokuwa
ndefu na nyeusi ti sasa zilibadili rangi na kuanza kuchipuka ovyoovyo.
Mdudu alikuwa ameniuma. Lakini yupi?
Darubini yangu ilinikumbusha mambo yalivyoanza. Yote yaling’oa nanga
baada ya kumaliza kidato cha nne. ‘Mrembo’ nilijidai kwenda jijini
kutafuta kazi ya ukarani. Niliwahakikishia wazazi kuwa nilikuwa na
rafiki wengi waliojitolea kunipa makao wakati nikitafuta kazi. Wavyele
wakadinda kuniruhusu mwanzoni lakini baada ya kuzidi kusisitiza na
kufanya kiburi nyumbani, waliafikiana na kuniacha kwenda zangu. Pengine
walikumbuka kuwa mtoto akililia wembe mpe. Nilipokuwa nikiondoka, mama
alikuwa na huzuni mno na kwa uchungu, alinionya kuwa mwenda tezi na omo
marejeo ni ngamani. Potelea pote. Sikutaka kusikia ya yeyote kwani
nilijitia hamnazo nisikie la mwadhini wala la mteka maji msikitini.
Nikawa binti kiziwi asiyesikia anayoambiwa.

Kazi baada ya kuikosa,nilijiunga na wenzangu na tukajiajiri wenyewe.
Malipo yakawa ya kuvutia ajabu kwani wateja walivyoongezeka ndivyo
malipo yalivyoongezeka. Alimradi ujue namna ya kuwaongelesha na
kuwahudumia wateja sawasawa. Jambo ambalo nilijifunza kufanya hata
nikabobea na kutopea katika nyanja hiyo. Waume niliwabadili kama
nilivyobadili mavazi yangu kwa siku. Nikawa ndiye jogoo la shamba
lililowika jijini. Nikazika katika kaburi la sahau kuwa jijini kuna papa
na papaupanga, ambao ukiwapapia, hukosi kupapatika kwa majuto, dhiki na
mateso kama hayo yaliyonikumba sasa. Lau kumbe mwiba wa kujidunga hauna
kilio.
Kutoka hapo uani nilikoketi, taa za umeme nilizoziona zilinikumbusha
mengi. Kuhusu mienendo yangu ya awali nilipokuwa kipusa ajabu. Niliingia
kwa vilabu hivyo vyote vya usiku huku mikono ya watu tofauti yamezinga
kiuno changu chembamba kama cha nyigu. Daima kucha zangu zilizokuwa
ndefu na zilinaksishwa rangi sawia na nguo zilizovalika. Mdomo wangu
ukakolezwa rangi nyekundu kana kwamba nililamba damu mbichi. Lakini
kumbe dunia mti makavu kiumbe usiuegemee.
Watu hao niliowatazama waliniongezea uchungu mtupu. Moyo wangu
mchanga ulijaa uchukivu na furaha ikawa imeyeyuka kama kipande barafu
katika utupu wa mchanga wa jangwa la Sahara. Wale wasichana warembo
waliovalia mavazi yaliyoacha sehemu za miiliyao kuonekana waliniudhi
zaidi. Laiti wangelijua kuwa dunia itawararua na kuwaacha uchiuchi,
wasingefika hata barabarani. Nilitamani kuwafikia niwaonye na kuwapa
ukweli wa mambo kuhusu madhara ambayo yangewasibu lakini nilishindwa.
Mimi pia nilikuwa hivyo na sasa nilikuwa naangamia. Nikakumbuka kuwa
asiyefunzwa na mamake hufunzwa na ulimwengu.
Waume nao niliwatazama kama wanyama mwitu waliovalia suruali ndefu na
sharti tofauti. Wanyama wenye uwezo mkali wa kukuvamia wakakumaliza
kabisa. Wao ndio walionipa maji machafu yaliyokuwa na mdudu ambaye
aliniuma na kunifanya kuugua sasa. Niliwatazama kwa uchukivu mwingi.
Raha nyingi ya ulimwengu ulitoweka na badala yake ikawa sasa ni
huzuni tupu na majuto. Sasa niliishi kwa jumba hilo kubwa peke yangu.
Ulimwengu ulinitenga kana kwamba mwenye ukoma. Wale wote waliokuwa
wakiingia na kutoka siku nzima hata usingewaona. Dada yangu mdogo ndiye
alijitolea kuniuguza pale kwani sikutaka kuishi na wazazi na kuwapa
mzigo wa kunitunza. Ikanijia kuwa mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.
Sikujua wa kumlaumu. Wazazi? La wao walinitakia mema na kunionya kusoma
kwa bidii. Marafiki? Kwa kiasi kidogo lakini ndimi niliyekubali
kudanganywa. Ulimwengu? Ndiyo lakini sehemu gani ya ulimwengu? Mimi
ndiye wakulaumu na sasa mwiba wa kujidunga hauna kilio.

Ndoto zangu zote zilitoeka kama ukungu na umande. Azimio langu la
kutaka kuendeleza masomo katika chuo kikuu katika fani ya sheria, na
kufuzu katika uzamifu na uzamili lilitoweka ghafla kama mwangaza wa
mshumaa uliozimwa na upepo. Nilitoka uani na kuingia katika chumba
changu cha kulala. Mezani, kulikuwa picha yangu ya awali.nilijiangalia
tena na kujiona tofauti; mnene, mwenye sura ya maji ya kunde tena
mcheshi ajabu. Lakini sasa nilikuwa kama shetani hata ingawa sijawahi
kuonana naye ana kwa ana. Haina maana kuishi katika hali hiyo!
Niliifikia kalamu na kuandika kitu kwa karatasi iliyokuwa hapo kando.
Kasha nikavuta kijichupa kilichokuwa hapo juu na kupiga makopo kadhaa ya
yaliyokuwemo. Maini ya kaanza kukeketeka na koo kuungua ndanindani.
Heri nife niiondokee dunia. Safari yangu ya kuenda jongomeoni ikawa
imeanza nilikolala sakafuni.
Niligutuka usingizini nikihema na kutweta kwa nguvu mno hata nikashindwa kuendelea kulala. Ilikuwa ndoto ya ajabu.
kisa kitamu tu sana na chenye mafunzo ajabu....... nimepende jinsi ulivyotumia methali katika kisa hiki. Heko kwako!
ReplyDelete